Wednesday, 17 April 2019

Ashatu Ageukia, baraza la wafanyakazi wa wizara ya fedha na mipango.






Baraza la wafanyakazi wa wizara ya fedha na mipango limetakiwa kufuatilia risimali fedha zinazotolewa kama zinatumika ipasavyo na kusimamia utekelezaji wa bajeti zinazotolewa na serikali kuhakikisha zinawafikia  wananchi wakawaida lengo likiwa nikujenga uchumi wa viwanda na kuchochea mageuzi ya uchumi na maendeleoa ya watu.

Hayo yamesemwa na naibu waziri wizara ya fedha na mipango dr.ashatu kijaji (mb) wakati akifungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa wizara ya fedha na mipango jijini Dodoma.

“”tunahitaji kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuziya uchumi wetu,maendeleo yetu sisi wanyewe pamoja na wananchi,hususani maendeleo ya watu wa kipato cha chini””

Aidha ashatu kijaji amelitaka baraza hilo kufanya kazi kwa ushirikiano,umoja,mshikamano,ufanisi na uadilifu pamoja na kuzingatia kanuni,sheria,taratibu na miongozo iliyopo katika wizara hiyo.

 “napenda kuchukua nafasi hii kusisitiza umuhimu wa kufanya kazi zetu kwa ushirikiano,umoja,mshikamano na ufanisi,tuzingatie sheria ,kanuni na utaratibu wa miongozo””

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi wa wizara ya fedha na mipango doto james amesema kuwa baraza hilo limeleta mafanikio mbalimbali ikiwemo kuboresha huduma kwa watumishi,kuboreshwa kwa mazingira ya kufanyia kazi ikiwemo kuwapatia watumishi vitendea kazi.

“”miongoni mwa mafanikio yaliyotokana na baraza la wafanyakazi la wizara yetu ni kuboresha huduma kwa watumishi na mazingira ya kufanyia kazi kwa kuwapatia watumishi vitendea kazi””

Nae naibu katibu mkuu wizara ya fedha na mipango dr.khatibu kazungu ameahidi kushughulikia suala la utoaji huduma bora kwa wafanyakazi hususani wasitafu ambao wanahitaji mafao yao ya usitafu.


0 comments:

Post a Comment