Saturday, 21 May 2016

Wadau waelimu wasema Serikali kupanga bajeti finyu kumechangia ongezeko la umasikini


Wadau wa elimu wanasema matokeo ya serikali kupanga bajeti finyu katika sekta ya elimu kumechangia ongezeko la umaskini na mgawanyo wa rasilimali usiokuwa na usawa katika jamii.
Mratibu wa mtandao wa elimu nchini TANMET Bi CATHLEEN SEKWAO amesema hali hiyo itaepukika  tu endapo serikali itaongeza  bajeti kwa ujumla hasa kwa watoto wenye mahitaji maalumu na waliopo katika shule jumuishi.
 
Alikuwa akizungumza katika maadhimisho ya wiki ya elimu duniani kitaifa yaliyofanyika Kilwa Masoko Mkoani lindi ambayo yaliyoambatana na maandamano yenye ujumbe mbalimbali.
 
Kwa upande wao wadau wa elimu wamesema takwimu zinaonyesha kuwa hali ya elimu nchini bado hairidhishi kutokana na takwimu kuonyesha bado kuna idadi kubwa ya watoto wa shule za msingi hawajui kusoma na kuandika.
 
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Ufundi  Mkaguzi wa Elimu wilaya ya kilwa TABU NASSORO amesema serikali inatambua mchango wa wadau wa elimu, taasisi na sekta binafsi katika kutatua changamoto za elimu nchini hivyo itaendelea kutoa ushirikiano.

0 comments:

Post a Comment