Saturday, 21 May 2016

mavuno ya zao la Mahindi yashuka kwa asilimia 4.3 Mkoani Njombe.

 

Mavuno ya mahindi katika Mkoa wa Njombe ambao ni miongoni mwa mikoa inayozalisha kwa wingi mazao yakiwemo mahindi unashuka kila msimu kutokana na matumizi ya mbegu bandia ambayo yamefikia asilimia na hivyo kuporomosha kwa uchumi wa mkoa huo.
 
Hayo yamebainishwa na matokeo ya utafiti uliofanywa na  Baraza la Kilimo na Mifugo Tanzania kwa kushirikiana na wataalamu kutoka chuo kikuu cha Daresalaamu  katika wilaya kumi hapa nchini.
 
Kwa mujibu wa Kaimu  Mkurugenzi wa baraza hilo CLEOPHAS RWECHUNGURA na mtaalamu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam KHALID FWADILI mkoani Njombe mavuno ya mahindi yanashuka kwa wastani wa asilimia 4.3 hali inayoporomosha uchumi wa  wakulima.
 
Katika mdahalo wa mbegu bandia Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Njombe ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Ludewa Bwana ANATOLY CHOYA amesema juhudi zinafanyika kupambana na wauzaji na waagizaji wa pembejeo bandia.

0 comments:

Post a Comment