Saturday, 21 May 2016

TANESCO ipo hatua za mwisho kukamilisha miradi mikubwa ya umeme ukiwamo wa REA.



Shirika la Umeme liko hatua za mwisho Mkoani Morogoro kukamilisha miradi mikubwa ya umeme, ukiwemo mradi wa umeme mijini na ule unaofadhiliwa  na mradi wa umeme vijijini REA ambapo zaidi ya watu 11,300 wanatarajiwa kufikiwa na umeme.
Hatua hiyo inakuja wakati Serikali ikielekeza nguvu zake katika mapinduzi ya Uchumi kupitia viwanda na huku fursa zaidi za kiuchumi zikiendelea kujitokeza kufanikisha azma hiyo mkoani kuchangia sekta ya viwanda.
 
Mhandisi wa umeme David  Chisot anayeshughulikia masuala ya Ujenzi na miundombinu ya umeme toka shirika la Umeme Tanesco Mkoa wa Morogoro, amesema kupitia miradi hiyo,wateja wakubwa na wadogo wataweza kufikiwa na nishati ya  umeme katika maeneo ambayo awali hayakuwa na umeme kabisa.
 
Chisot amesema miradi inayofadhiliwa na REA inayogharimu  itahusisha wilaya 4 katika  mkoa wa Morogoro ikiwemo Morogoro katika vijiji 27 , Mvomero  vijiji 35, Kilombero vijiji vinne na Ulanga vijiji 5 vitano ambapo tayari  wateja 5,562 wa mradi wa REA wameanza kunufaika na mpango huo wakiwemo wateja wadogo 5457 Na wakubwa 205.

0 comments:

Post a Comment