Mkoa wa
Dodoma umepanga mikakati kwa kila mtu kufanya usafi katika makazi yake na mita
5 kuzunguka nyumba yake pamoja na taasisi zote katika mkoa huo lengo likiwa ni
kuboresha mazingira ya mkoa huo na kuendelea kushika nafasi bora za usafi
kitaifa.
Hayo
yamesemwa na afisa afya wa mkoa huo Kali Sailas Lyimo katika mkutano
uliofanyika wa wadau wa usafi wa vyoo na mazingira mkoani humo wa kujadili
mikakati ya uboreshaji wa mazingira wa mkoa huo.
Kwa upande
wake mratibu wa kampeni ya usafi wa mazingira mkoa wa Dodoma francis muliku
amesema kuwa mkoa wa Dodoma umekuwa na mafanikio makubwa sana ya usafi wa
mazingira ambapo idadi ya kaya zenye
vyoo bora imeongezeka katika mkoa huo.
Nae mratibu
wa afya shule za jiji la dodom mwalimu theresia mudaha ameelezea changamoto za
vyoo zilizopo katika jiji hilo na kusema kuwa usafi wa mazingira shuleni ni
mzuri katika jiji hilo.
Afisa afya
wa halmashauri ya wilaya ya chamwino Kathibeti kongola amesema kuwa katika
halmashauri hiyo ya chamwino idadi ya nyumba zenye vyoo imepanda kutoka
asilimia 81% hadi asilimia 99.62 katika halmashauri hiyo.







0 comments:
Post a Comment