Tuesday, 26 March 2019

Tanzania kuokoa kiasi cha dola za kimarekani milioni milioni 206 kwa mwaka au 1% ya GDP.



Takriban asilimia 60 ya watu wamefikiwa na huduma ya maji safi na salama ,huku asilimia 46.24 wakifikiwa na kiwango cha vyoo bora vilivyoboreshwa.

Taarifa hiyo iliyojiri juma lililopita wakati wa kilele cha wiki ya maji na imefafafanua kuwa idadi ya watu inakua kwa kiasi kikubwa na kuzidisha athari zitokanazo na  upungufu wa huduma za usafi wa mazingira.

Hata hivyo mahitaji ya maji katika secta za uzalishaji  mf.umeme ,kilimo ,utengenezaji wa viwanda yanakuwa kwa kasi kadiri uchumi unavyokuwa na hivyo kutajwa kuwa secta hiyo itaendelea kukua iwapo msukumo ukiwekwa kwenye rasilimali  hiyo ya asili kwa kadiri idadi ya watu inavyokua.

katika dhamira ya hakuna anaye achwa nyuma ,serikali ,secta binafsi ,taasisi za kitaaluma na asasi zisizo za kiserikali hukutana kubadilishana ujuzi ,kutathimini ufanisi na kuandaa ufumbuzi wa changamoto zinazohusiana na maji katika juhudi za kuhakikisha hakuna yeyote anayeachwa nyuma.

Aidha,Huduma za usafi zilizoboreshwa zimetajwa kuifanya Tanzania kuokoa kiasi cha dola za kimarekani milioni milioni 206 kwa mwaka au 1% ya GDP.


Taarifa hii inajiri wakati ambapo ni siku nne zimepita tangu Tanzania kuungana na nchi nyingine duniani kuadhimisha wiki ya maji ,ambapo kitaifa maadhimisho hayo yamefanyika jijini Dodoma

0 comments:

Post a Comment