MAMLAKA ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) imetoa notisi kwa
wapangaji wa nyumba zake 174 zilizopo Kikuyu Mjini hapa ambazo ni za ghorofa
mbili kuhama ili kupisha ukarabati mkubwa wanaotaka kufanya.
Akizungumza jana Ofisa habari
na mahusiano wa CDA, Angela
Msimbila alisema, walishatoa notisi ya siku saba ya kuwataka wapangaji wote
kuhama ili kupisha ukarabati mkubwa unaotakiwa kufanyika kwenye nyumba hizo
ukiwemo wa majengo, mifumo yote ya umeme, vyoo na majitaka.
Amesema awali wapangaji hao walikuwa wakilipa kodi ya Sh.
18,000 kwa nyumba yenye vyumba viwili na sebule, kodi ya Sh 20,000 kwa nyumba
yenye vyumba viwili, sebule na sehemu ya kulia chakula, kodi ya Sh 22,000 kwa
nyumba ya vyumba vitatu, sebule na sehemu ya kulia chakula.
Hata hivyo mwaka 2008 mamlaka hiyo ilifanya mabadiliko ya
kodi za nyumba katika maeneo mbalimbali
ikiwepo nyumba za Maghorofa ya Kikuyu, mabadiliko hayo yaliongeza viwango vya
kodi katika nyumba hizo kwa kuzingatia uwiano wa kodi katika soko.
Amesema ongezeko hilo la kodi lilitaka wapangaji kulipa kodi
kati ya Sh. 50,000, Sh,55,000 na Sh. 65,000 jambo ambalo hawakukubaliana nalo
na kwenda kufungua kesi mahakamani
“Baada ya ukarabati kodi katika nyumba hizo zitapanda na kuwa Sh, 120,000, Sh130,000 na Sh l50,000
na wapangaji watakaokuwa na vigezo watapangishwa nyumba hizo na mamlaka”
alisema
Msambira alisema mwaka 2008 wapangaji walipeleka kesi
mahakamani (Baraza la Ardhi) kupinga kupandishwa kwa viwango vya kodi na kesi
hiyo ikaanza kusikilizwa.
Amesema tangu kipindi hicho kumekuwa na mwendelezo wa kesi
mbalimbali za kupinga ongezeko la kodi mpaka mwaka 2016.
Alisema kutokana na kesi hizo wapangaji zaidi ya 150 waligoma kulipa kodi tangu
wakati huo na kuisababishia mamlaka hasara kubwa.
Msimbila alisema CDA imekuwa ikikusanya kodi jumla ya Sh. Milioni
3.4 kwa mwezi bila kodi ya ongezeko la
Thamani(VAT) na ukitoa kodi hiyo mamlaka imekuwa ikipata Sh. Milioni 2.9.
Alisema mamlaka hiyop imetenga fedha za ukarabati wa majengo
hayo katika mwaka wa fedha 2015/2016, ilitangaza zabuni na kumpata mkandarasi
wa kufanya ukarabati.
Alisema kwa sasa
mamlaka hiyo imejipanga kufanya zoezi la kuwaondosha wapangaji watakaokaidi
ilani ya kuwataka kutoka ndani ya siku saba kwa kutumia dalali.






0 comments:
Post a Comment