Friday, 8 March 2019

Mfumumuko wa bedi ni asilimia 3.0


OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia februari  2019 umebaki kuwa asilimia 3.0 kama ilivyokuwa kwa mwaka ulioshia Januari 2019.
Hiyo ina maanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa Februari mwaka huu imebaki sawa na kasi iliyokuwepo Januari mwaka huu hivyo kusababisha mfumuko wa bei kubaki asilimia tatu.
Akizungumza leo jijini Dodoma  Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Kijamii EPHRAEM KWESIGABO amesema mfumuko huo wa bei kwa mwezi Februari mwaka huu umebaki sawa kama ulivyokuwa Januari mwaka huu.

Amesema mfumumo kubakia hivyo hivyo ni kutokana na kuongezeka na kupungua kwa baadhi ya bidhaa za vyakula na visivyo za vyakula na kutaja baadhi ya vyakula vilivyopungua bei kwa kipindi cha mwezi februari 2018 mpaka februari 2019.
KWESIGABO amesema mfumuko wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa Februari mwaka huu, umepungua hadi asilimia 0.5 kutoka asilimia 0.7 ilivyokuwa Januari mwaka huu.
Akizungumzia hali ya mfumuko wa bei kwa nchi za Afrika Mashariki amesema  Uganda mfumuko wa bei kwa Februari mwaka huu umeongezeka asilimia 3.0 kutoka 2.7, Kenya umepungua hadi asilimia 4.14 kutoka asilimia 4.70 kwa mwaka ulioishia Januari mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment