MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Amanda Poshi amefungukia taarifa zinazomhusisha yeye kuugua maradhi ya Ukimwi.
Amanda amefunguka hayo baada ya kuvuja kwa picha zake zinazomuonesha
akiwa amepungua mwili na kusababisha gumzo litawale kwenye mitandao
mbalimbali ya kijamii watu wakihusisha kukonda kwake na ugonjwa huo
ndipo mwanahabari wetu alipombana, akafunguka:
“Nina desturi ya kupima kila wakati, hawanipi presha. Nimeshapima
mwaka 2013 kibao na mara ya mwisho ni mwaka jana lakini hayo madai
yamekuwa yakiibuka mara kwa mara wananiboa kweli mbaya zaidi hao
wanaolazimisha nipime wao wenyewe hawapimi. amanda
“Nilipokuwa mnene presha ilikuwa inashuka kila mara, namshukuru Mungu
kwa sasa nimeanza gym niko imara, nimepungua mwili vizuri.”
baada ya kusema hayo Amanda alimtumia mwanahabari wetu vyeti vyake mbalimbali vyenye majibu ya Ukimwi vikionesha yupo safi
0 comments:
Post a Comment